Tuesday, November 26, 2013

James Maina Atua Musoma Information Center Kuleta kitu kipya

James Maina Kutoka Nairobi kenya akiwa ni Mwalimu mzoefu wa mambo ya Design akitokea katika shirika la Nairobits School of Digital Design( www.nairobits.com).Alipewa nafasi ya kuweza kuwatembelea wanafunzi wa Musoma Information Center ambacho ni chuo kinachofundisha mambo ya webdesign and Programming kwa lugha ya kitaalam kuweza kuwaletea kitu kigeni katika mafunzo yao. Alikuja Musoma kwa ajili ya kuwafundisha vijana kitu kigeni kinaitwa "Information Architecture". na "Design/Creative thinking".

Kiukweli hapa vijana walipata nafasi ya kuweza kujifunza mambo muhimu sana ambayo wanatakiwa kuyafanya wanapokuwa wamewapata wateja wao wa kumtengenezea tovutu ( website)
Vijana walipata kujua ni jinsi gani anaweza kuongea na mteja wake na pia walipewa mwanga juu ya vitu ambavyo mteja wake anafaa kumpatia ili aweze kumtengenezea tovuti.
Pia walielekezwa jinsi gani wao kama web designer wanaweza kukaa chini na kupangilia mfumo mzima wa tovuti itakavyokaa na kuendana na hitaji la mteja wake.

JAMES MAINA akiwa katika maandalizi ya kipindi maana hakuna jambo zuri ambalo litafanyika bila maandalizi
Wanachuo wa Musoma Information Center walipomapata ujuzi huo kutoka kwa bwana James Maina ilifikia wakati wa kuanza kufanya kwa vitendo na kama unavyoona katika picha hawa ni baadhi ya wanachuo wakiwa katika zoezi la kuonesha ni nini wamejifunza kutoka kwa Bwana James.
Mmoja kati ya wanachuo waliopata mafunzo hayo akijulikana kama " Uyanjo Yakobo" akijaribu kuweka maelekezo aliyoyapata katika karatasi hatimae ayahamishie katika computer.

Ushirikiano katika kusoma ni jambo la kujenga sana, kwa sababu ukileta nilichokipata na mimi nikaleta changu tunakuwa na kitu kizima tuliokanyaga umande tunalitambua hilo.
Baada ya majadiliano twende kazi sasa kutoka kushoto Janepha Nassoro, Victor Mandara na Shekha Khamisi wakiwa katika harakati za kutaka kumwonesha Bwana James Maina kuwa safari yake kutoka Nairobi Kenya Hadi Musoma Tanzania haijaenda bure kuna kitu kweli kaleta.